Friday, April 19, 2013

BMU NI WASIMAMIAJI WA RASILMALI ZA ZIWA AU WATAWALA ?


            

Vikundi vya kusimamia rasilmali za ziwani maarufu kama BMU ni vikundi vya wadau vilivyoundwa kisheria kwa dhumuni la kusaidiana na Serikali katika zoezi zima la kuhifadhi mazingira ya mialo,kushirikisha wavuvi katika kuhakikisha kuwa rasilmali zote za  samaki zinahifadhiwa kwa manufaa ya taifa.

Vikundi hivi kulingana na malengo ya kuanzishwa kwao yalijikita katika kuhakikisha ufuatiliaji endelevu wa kudhibiti uvuvi haramu unakuwepo na hivyo endapo zoezi hilo lingefanikiwa uchumu wa taifa ungeliimarika hususan bidhaa yote itokanayo na samaki iwapo  ingelipitia katika utaratibu mzima wa kiserikali.

Aidha huenda pengine nao wahusika katika kuhakikisha kuwa shughuli za vikundi hivyo hawana mwanga wa kutosha ya kwamba wao inawabidi wafanye nini ndio maana kazi zao zinaonekana hafifu kiasi kuwa uvuvi huo haramu unaonekana kushamiri katika baadhi ya mialo ya kanda ziwa.Uendelevu wa kuwepo kwa zana haramu za uvuvi katika vijiji vya wavuvi ni jambo linaloonyesha ulegevu wa wazi wa vikundi vya BMU.

Huenda pengine serikali haijui kwa undani ni kwa vipi vikundi hivi licha ya kuwezeshwa kikazi na kimaadili lakini bado wanakwepa wajibu na kuviacha viwanda vya samaki vikanyang’anywa mali ghafi hadharani  na huku zikielekea wakati mwingine katika nchi jirani.Nchi hii ni yetu ni wajibu serikali yetu ikashauriwa na kutahadharihwa kwa hili.

Vikundi vya BMU inabidi viendeshwe kwa kuzingatia kanuni zake na viongozi wake kuzigatia mapashwa yao ambayo ni kuwa kama mawakala wa serikali atika upande huo wa uimaishaji wa uchumi wan hi yetu.

Kinyume na hayo viongozi wengi katika mialo mbalimbali wameachana na makusudio ya wajibu wan a kujiingiza katika mambo kiutawala,kuamua mashauri ya wakazi wa maeneo yao hata kama mashauri hayo  hayahusiani kamwe na masuala ya ziwani kama vile magomvi ya kifamilia,kutoza tozo za mashauri hayo,kunyan’anya ardhi,kuwanyanyasa wananchi au wavuvi kwa kuwafukuza katika makazi yao,kuharibu mazao yao hasa iwapo mhusika ameonyesha kutokukubaliana na utaratibu wa viongozi hao. Hivyo muda mwingi unaishia katika mambo ya kiutawala.

Kanini za BMU zinaeleza wazi kuwa vikundi hivyo vitafanya kazi chini ya uongozi wa Serikali za vijiji au mitaa ziliko.Kwa hali halisi ilivyo kanuni hizo ni ndoto kwani viongozi wa vikundi hivyo wamekuwa wakijiingiza katika kuwadharau viongozi wa vijiji na kujifanya wao kuwa watawala.Vurugu nyingi zimekuwa zikibainishwa katika kambi za wavuvi viongozi wa vikundi hivyo wakijifanya miungu.

Taratibu za aina hiyo ndicho chanzo cha ukwamishaji wa shughuli za usimamizi na ufuatiliaji wa wavuvi haramu na wao kushindwa kuripoti vitendo hivyo serikalini na kwa wakati na hivyo kuwepo kwa takwimu za ubabaishaji za doria zilizoendeshwa.K
a.
.Kusimamia miradi midogo midogo ya kiuchumi kwa manufaa ya jamii ya wavuvi.
.Kuendesha doria za mara kwa mara dhidi ya uvuvi harramu.
Kwa upande mwingine kanuni hizo zinataja dhahiri kuwa chini ya Sheria za Serikali za mitaa Na.7 na 8 za mwaka 1982,vikundi hivyo vitaundwa kama vikundi vingine katika kijiji au Mtaa na vitaendesha shughuli zake chini ya serikali hizo za vijiji au mitaa.
Tofauti na muongozo huo wa vikundi vya BMU baadhi ya viongozi wa vikundi hivyo wanaacha kuendana na wajibu wao badala yake wanabaki kusigana na Halmashauri za vijiji juu ya mambo ya kiutawala.

Saturday, March 30, 2013

Kagera Looks Ahead



KAGERA LOOKS AHEAD




Source or Author: William Oswald Rutta- Operations Manager – kiroyera Tours @2013.

KAGERA:  The name of one of the two large rivers and which Kagera region is named. This is the real source of River Nile the longest river in the world.
Kiroyera tours a pioneer tour operator for more than a decade now have been operating mainly on cultural tours, safaris to Tanzanian National park, and trip to Uganda for Gorrilla tracking

Tourism wise, Kagera is in Tanzania located between four natural African wonders that isGorillas in Uganda and Serengeti in Tanzania Serengeti,Ngorongoro and Kilimanjaro. Kagera region lies on the border with several neighbouring countries all hosts to individual tourist attractions. These include Uganda and Rwanda Gorilla trekking and Kenya’s well-developed tourism.

Kagerahas many unique attractions that stand to provide diversity to the Tanzania tourist attractions. The challenges we have not been able to utilize the same as we have few tour operators known much about it. KIROYERA TOURS  (www.kiroyeratours.com) is a leading tour operator for more than a decade now, other tour operator is WALKGARD HOTEL AND TOURS  and good number of hotel.
The tourist attractions contribute can contribute to the economic well-being of the region, improvement of social infrastructure, creating jobs and income for the local population. Attractions include; pleasant weather, Lake Victoria its size is equal to Ireland,the largest fresh water lake in Africa with its attractive islands and spectacular white sand beaches, and have potential to provide many water-based leisure activities. There is Kagera River, the source of the Nile which is the longest River in the World, wildlife protection areas and exceptional bird watching sites a strong culture based on well-run small Kingdoms documented to the 14th century. This area has unique biodiversity seen in endemic species of flora and fauna and unique landforms such as numerous inland lakes and a long eventful history of explorers, the slave trade, religions, business groups and ancient rock art. Not only that but also game reserves to mention few Biharamulo, Burigi, Ibanda game reserves, water falls, Mutagata hot spring, caves, Rubondo Island National park a paradise for bird lovers and spot fishing.  Kagera is between the Gorillas and the Serengeti both world class attractions and the region is between five cities including Kampala, Kigali, Bujumbura, Nairobi and Mwanza. All within reach in less than a day of surface travel. This gives it potential to be a major supply center.
Bukoba originated from clan known as BAKOBA which is the administration headquarter of Kagera Region.Bukoba is a small bustling typical Africa town with an attractive waterside setting with about 100 years old. Is the best for you to do a community walk through Bukoba town, the town is very clean with weekly cleaning campaign from the Regional Commissioner Carnal Fabian Massawe,   you will visit the local marketwith varieties of food, bananas, fresh fruits, garments, a school, a church, the museum and a wood workshop operated by disabled people.  Night life is available at Linus night club, good hotels, security is assured and clubs including giant Rotary club of Bukoba.
The local product has been improving, particularly the infrastructure, including transport by air (precision air, Auric air, fly 540) all connect to Bukoba to Dar essalaam,Nairobi, Entebbe, Kigali, and to Eurpe and America, main road are all tarmac road, water and air communication is easy with e-mail, Vodacom, zanteltigo,  banks with MasterCard service, ATM, min supermarket and good telephone systems. Trade is liberal and currency transactions are easy, plus expert tourists center visitwww.kiroyeratours.com focused hotels to mention few Walkgard Hotel, Victorious perch, Smart hotel, kolpinghotel,Baramaga bed and breakfast, ELCT Bukoba hotelaned camping site on shore of Lake Victoria managed by Kiroyera Toursand other many are springing up in Bukoba regularly.
Are you looking for investment? Kagera is the place to invest- we have constant supply of electricity, fertile land for agriculture, politically stable and evergreen with pleasant climate. We look to have some company who can also invest in sports (soccer for men and women) promotional of traditional games (wrestling, Bao, Omutoro, spare throwing etc.)
Kiroyera tours has organized the tour to Rubondo Island being promotional tours to local Tanzania in celebration of world tourism day to support the 2012 theme of UNWTO ‘ Tourism and Sustainable Energy’


Kiroyera tours  means turn dark bright
Our Mission
To widely promote Lake Victoria in particular Kagera Region as a Tourist Destination, focus on community based tourism and operate quality assured tourism services within the Lake Region and beyond.

"Trough our consultancy services, to contribute to capacity building and ensuring Kagera and other areas of Tanzania make the most of their Natural assets now and for the future"

Our vision
Kiroyera Tours will remain a leader in Tourism Development for the Lake Victoria Region by sustaining a high rank among the best companies and a preferred choice for tourists and other clients. We have attended mora than 5000 tourist since for last ten years and main destination is cultural tours, boat and flight tickets, safari to Tanzania national park, community tour and Gorillas in Uganda

KageraAmaninamaendeleo!!
@William Oswald Rutta March2013.

SENENE HISTORY



Kwa kutumia vyanzo mbalimbalina imekuzwa na William Rutta – Kiroyera tours www.kiroyeratours.com

KUNA aina nyingi za wadudu ambao katika baadhi ya makabila hapa nchini hutumiwa kama kitoweo,na pia katika uzalishaji wa bidhaa za vyakula kwa ajili ya matumizi mbalimbali.
Senene ambao hupatikana kwa wingi mwishoni mwa kila mwaka, ni miongoni mwa wadudu wanaotumiwa zaidi na kabila la wahaya mkoani Kagera kama kitoweo, pengine kuliko kabila jingine unalolifahamu.

Hata hivyo pamoja na kitoweo hiki kupewa heshima kubwa na hata kuwa sehemu ya mila na utamaduni wa kabila hili,asili na chanzo cha senene limeendelea kuwa swali gumu miongoni mwa wenyeji wa mkoa huu.

Wahenga walisema ‘uzee dawa’na katika kutafuta majibu ya siri ya senene katika kabila hili,safari yangu ilinikutanisha na mzee David Zimbihile(80) aliyekuwa mbunge wa kwanza wa jimbo la Ihangiro sasa ni Muleba Kusini.

Wakati wa uongozi wake alikuwa na mvuto mkubwa kwa wapiga kura,na hadi leo anakumbukwa kama kiongozi ambaye utawala wake ulikuwa na baraka za wingi wa senene kila mwaka.
Anasema katika moja ya kampeini zake aliwahi kulalamikia kukosekana kwa mboga,na badala yake aliomba senene .Sara zake zilisikika na kuanzia wakati huo wananchi wakaendelea kumwamini huku madai ya uwezo wake wa kuleta senene yakitumika kutetea nafasi yake.
Mzee Zimbihile anasema pamoja na kupata umaarufu kupitia kitoweo cha senene miongoni mwa wapiga kura,anasema hakuwa na uwezo huo na kudai aliwaomba na Mungu akasikia sara zake kutokana na uhaba mkubwa wa mboga uliokuwepo wakati huo.
Hata hivyo pamoja na kusema senene ni kitoweo kinachoheshimika bado hakuweza kufahamu asili yake na sababu za wadudu hao kuvutiwa na mazingira ya mkoa wa Kagera katika misimu miwili kwa mwaka.
Anaamini ni uwezo na mapenzi ya Mungu,huku akikumbuka wakazi wa eneo la Bunya katika nchi ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) walivyomshanga wakati alipokuwa wanakamata na kula senene enzi hizo akifanya kazi nchini humo.
Maswali yangu hayakupata majibu na alihitimisha mazungumzo kwa kusisitiza kuwa tamaa ya kula senene iliwafanya wanaume kuwaongopea wanawake kuwa kama wangekula kitoweo hicho kingeweza kuwadhuru.
Hata nilipozungumza na Saida Sarehe(67)mkazi wa eneo la Kashai mjini hapa,alidai hakuna historia yoyote kwenye kabila lao inayoeleza chanzo na asili ya wadudu hao na kudai Mungu aliitoa kama neema kwa wakazi wa mkoa huo.
Ni muuguzi mstaafu ambaye anaishia kunisimulia jinsi wasichana wa enzi zao walivyopeleka senene kwa wachumba wao,ambaye hakufanya hivyo ilimaanisha uwezekano wa kuolewa na mchumba wake ulikuwa mdogo.Senene walitumika kama ishara ya upendo na uaminifu.
Anasema hawakuruhusiwa kula senene na kudai vitisho vya wanaume vilivyojificha kwenye tamaa na uroho wa senene viliwafanya wale kitoweo hicho kwa siri kubwa.
Bila kunipa majibu ya maswali yangu,analalamikia ubabe wa wanaume uliowakataza kula vitu vitamu na kuanzia hapo ananipa siri ya eneo la mkoa huu kuitwa Buhaya. Kuna baadhi ya vitu vitamu vingine kama kuku, nyama ya mbuzi, mayai wakina mama hawakurusiwa kula. Wazee wa kihaya kimila walidai mwanamke alikuwa haruhisiwi kutmumia vile kizazi kilikua shida na kwa kutumia mayai, nyama ya mbuzi na kuku wangenenepa na kushindwa kuzaa kwa wepesi ikawa ni mwiko, Bibi yangu Felista Nyamwiza aliyafariki mwaka 2010 akiwa namika 88 hakuwahi kula senene, yai wala kuku katika maisha yake yote pamoja na kutuandalia senene sisi wajukuu zake.
Kwamba wanawake walionywa wawe na haya siku zote, na wasivunje mwiko kwa kula vitu walivyokatazwa.Wote walikuwa na utii wakiheshimu mila na desturi za kabila lao.Walifundishwa kuwa na haya wasichana wa Buhaya.
Hata Khadija Khalphan(84)mkazi wa Kashai mjini Bukoba mbali na kufahamu umuhimu na nafasi ya kitoweo cha senene katika mila za kabila lake anakiri kutofahamu chanzo na asili ya wadudu hao.
Hata mvua za vuli zinazoanza mwezi Novemba ambazo huambatana na ujio wa senene ,msimu huo hutambuliwa na wenyeji kwa jina la mvua za Omusene ikiwa na maana halisi ya mvua za msimu wa senene.
Pamoja na senene kuwa ishara ya neema katika kabila hili,pia inadaiwa ni dalili za kuwepo tukio baya endapo mtu ataota kuona senene wengi.
Juhudi za kufahamu siri ya senene zinanifikisha katika kituo cha Utafiti wa Kilimo Maruku,na baada ya kushindwa kumpata mtaalamu wa sayansi ya wadudu niliamua kutafuta majibu kwenye vyanzo mbalimbali kwenye mtandao wa intaneti.
Zipo aina nyingi za senene ambapo wale ninaowazungumzia wamegawanyika katika kundi lijulikanalo kwa kitaalamu kama Orthopterous na huzaliana kwa wingi katika mwambao wa maziwa makuu,baada ya kutaga mayai yao ardhini kipindi cha kiangazi.
Baada ya kutaga mayai na kuanguliwa,mzunguko wa maisha yao huisha kati ya mwezi Octoba na Desemba ambapo huruka wakiwa katika makundi makubwa wakihitimisha safari ya maisha yao.
Senene hao ambao wako katika jamii ya nzige pia hutofautiana kutegemea mazingira yaliyopo na hali ya hewa, na tangu zamani hupenda kuweka makazi yao juu ya vilima.
Kwa mujibu wa vyanzo vya mtandao katika nchi ya Japan senene wa kijani humaanisha dalili njema,na mwanzo mzuri wenye matumaini ambapo pia hutumika katika utengenezaji wa chokoleti.
Hii ni aina ya panzi wapole ambao hawana tabia ya kuharibu mazao na kuteketeza makazi yao kwa chakula kama walivyo jamii ya nzige.
Hawa ni aina ya panzi ambao baada ya kuzaliana, maisha yao ya mwisho hupenda kuyamalizia kwenye ukanda wa kijani na bila shaka mkoa wa Kagera ukiwa ni chaguo bora zaidi.
Senene huanza safari yao wakati wa giza huku pembe zao zikiwa zimeangalia chini na mara waonapo mapambazuko hujificha chini kwenye nyasi.
Pengine ndiyo sababu wafanya biashara wa senene hufanikiwa kuwahadaa kwa mwanga mkali wa taa,na mara kadhaa makundi makubwa ya senene huletwa na mawimbi ya maji baada ya mapambazuko kuwakuta kwenye maeneo ya ziwa Viktoria.
Senene hupatikana mahali pengi duniani ingawa hutofautiana kutokana na mazingira na ikolojia ya eneo hilo.Madume hutoa mlio maalmu kuwavutia majike ingawa pia milio hiyo hutofautiana kutokana na aina ya senene na kundi lake.
Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Chakula na Kilimo duniani(FAO)ya mwaka 1999 katika utafiti wake wa ‘Non-wood Forest Product in Tanzania’umebainisha kuwepo kwa wadudu wengi wanaotumika kama kitoweo katika maeneo mbalimbali hapa nchini wakiwemo senene.
Utafiti huo pia unawataja wadudu kama kumbikumbi,swah,nywa na fihwa kuwa mbali na kutumika kama kitoweo pia huzalisha mazao mbalimbali ya chakula.
Hata hivyo senene na aina ya moja ya mchwa warukao wanatajwa kuwa na umuhimu mkubwa katika misitu ya miombo na kuwa wdudu wote hawa huuzwa katika masoko ya ndani baada ya wekewa chunvi na kukaangwa vizuri.
Katika miaka ya hivi karibuni safari ya senene kuelekea mashambani hufupishwa na wafanyabiashara ambao huwekeza pesa nyingi na kuwatega kwa kutumia taa zenye mwanga mkali.Katika eneo la Nyamkazi mjini Bukoba gharama ya kukodi eneo la kuweka mtego wa senene sio chini ya shilingi laki moja na waachuuzi wadogo humlipa ‘mwekezaji’shilingi elfu moja ili waruhusiwe kuokota senene watakaoanguka nje ya pipa lililofungwa taa.
Kwa vyovyote vile changamoto za mabadiliko ya tabia nchi na ushindani wa kibiashara utakifanya kitoweo cha senene ambacho ni sehemu ya utamaduni wa Wahaya uanze kusahaulika na pengine kubaki kwenye historia tu.
Senene kwa sasa imekuwa ikitumika kama kitega uchumi na hajira ya iana mbili. Kuna ajira ya kundi la Vijana wa Muda na Ajira ya kudumu kwa baadahi ya wajasiamari. Ajira ya muda ni kwa vijana hata ambao sio wahaya wamekuwa wajikiika katika kuwakamata na kuwauza wakati wa msimu tu na kundi la pili ununua senene nyingi amabazo uuzwa kidogo kidogo hadi msimu wa pili unapoanza. Senene zimekuwa zikitumwa kwa njia ya bus, ndege kwa wahaya walioko ndani na nje ya Tanzania hadi huko famle za kiharabu, marekani, ulaya, austaria, Africa kusini na hata Brazil na kuogeza pato kwa wakazi wa Bukoba. Ukweli senene ni wadudu wanaongeza urafiki mkubwa kwani akitumiwa mtu kama zawadi anaweza kukuleta na kukujibu kwa zawadi kubwa mara dufu mfani senene za elfu tano ukimtumia rafiki mpendwa aliye ulaya anaweza kukutumia ngua kama suti yenye dhamaniya zaidi yalaki nane!!
Mazingira yatunzwe vizuri ili wanedlee kuleta neena mkoani kwetu
By William Oswald Rutta
Manager- Kiroyera Tours @2013

TALII UTAUINUA UCHUMI MKOANI KAGERA



(Na Gilbert J Makwabe)
Fursa za utalii katika mkoa wa Kagera zimebainishwa kuwa nako zipo ambapo baadhi ya watalii wan je na ndani ya nchi wanaonekana kuutembelea hususan wale wa kutoka nchi mbali mbali duniani.

Mkoa wa Kagera ukiwa ni mkoa pekee unaopakana na nchi zote za Africa Mashariki na nchi za maziwa makuu ni hazina kubwa ya nchi ya Tanzania.Mkoa huu umeshuhudiwa kuwa miongoni mwa mikoa yenye hali nzuri ya hewa,mvua za kuaminika,hali nzuri ya uoto wa asili ambapo karibu kila majira ya mwaka uoto wake hubakia ni wa kijani.Kwa hali hiyo ni vigumu sana kuutofautisha mkoa huo na majimbo kama vile Cape town la Afrika Kusini au Rift Valley la huko Kenya kwani ni hali ya kiubaridi baridi na joto la kadiri.Huo ndio mkoa wa Kagera na Mwenyezi Mungu ndivyo alivyouumba mkoa huo.

Tukizirejea taarifa za hivi karibuni kutoka Mamlaka ya Hali ya Hali ya Hewa Tanzania zimeonyesha kuwa kipindi cha mvua za vuli mwaka 2010/2011 ziliongezeka kutoka milimita 80.7 mwezi Augusti 2010 hadi kufikia milimita211.1 mwezi Desemba 2011 sawa na wastani wa milimita 173.42 kwa mwezi. Aidha kwa kipindi cha Januari2012 hadi Mei 2012 mvua ziliongezeka kutoka milimita 94.3 kwa mwezi hadi kufikia milimita 298.18 kwa mwezi.

Taswira hiyo inatuweka katika dhana ya kuwa mkoa kweli unayo matarajio mazuri kwa upatikanaji wa chakula cha kutoasha kwa wananchi na watalii pia,upatikanaji wa maji ya kutosha,malisho ya mifugo na wanyama pori pia. 

Dhana ya utalii mkoani humo imeibuliwa sio muda mrefu uliopita kama mwaka 2002 ambapo kampuni moja ijulikanayo kama Kiroyera tours ilianzishwa kwa madhumuni ya kuanzisha shughuli za kitalii mkoani humo,Tanzania na Afrika Mashariki.

JE,UTALII NI NINI?
Hatuhitaji kukuna sana vichwa kwa kujiuliza swali hilo utalii ni utamaduni wa kutoka sehemu moja na kuitembelea sehemu nyingine,na kwa maana ya utalii katika mada hii nikuwa ni sharti afikiriaye kutalii ajipange kifedha kwanza! Na mtalii huwa na mambo yanayomfanya aweze kutalii,navyo huitwa ni vivutio.Zipo aina nne za vivutio navyo ni VIVUTIO ASILIA ambavyo ni hifadhi za taifa,mkao wa nchi na hali ya hewa.VIVUTIO VILIVYOTENGENEZWA kama mahoteli makubwa,kambi rasmi kwaajili ya wageni,mialo kando ya ziwa au mito,mashamba makubwa kama yale ya miwa,chai majengo mazuri.MATUKIO kama vile uchaguzi mkuu(waangalizi wa kitaifa na kimataifa).AMANI ya nchi.

Ni dhahiri vivutio viingi havijaainishwa mkoani humo lakini vipo ambavyo tayari vimeainishwanavyo ni kama vile Ziwa kongwe kabisa VICTORIA NYANZA upande wake wa magharibi na mialo yake iliyo na maeneo mazuri kabisa ya mchanga mweupe,ukarimu wa wananchi,kisiwa cha Nabesiga,Maeneo ya hija kama vile Nyakijooga,Kishomberwa,msitu wa hifadhi ya taifa Minziro,Uwanja wa mashujaa wa vita vya  

Maeneo mengine ambayo hupendelewa na watalii wafikao mkoani humo ni pamoja na jumba la makumbusho la Bukoba,maporomoko ya maji,Kyamunene hapo pia kuna pango lenye kuhifadhi popo wa ajabu ambao ni nadra sana kuwakuta sehemu nyingine.Hifadhi katika pori la Keza wilayani Ngara,Hifadhi ya wanyama pori ya Biharamulo,mbuga ya wayama Burigi ndani ya mapori hayo wapo wanyama wajulikanao kama  STATUNGA(kama swala)na hawpatikani popote,na wapo pia aina Fulani ya tumbili ambao wataalamu wa wanyama pori wanasema kuwa walitokea nchini Kongo . Mkoa huo pia unamiliki mapori yanayootesha miti ya michongoma na jamii ya miti ijulikanayo kwa kitaalam kama’acacia’ inayopendwa sana na wanyama pori.

Alipohojiwa na mwandishi wa makala haya kuzungumzia juu ya sekta ya utalii mkoani Kagera Meneja wa operesheni za utalii wa hoteli maarufu ya kitalii katika manispaa ya Bukoba,THE WALKGARD HOTELS AND TOURS Bw.Mugashe Leonidas alisema,’utalii ni hobby’ au hulka ya mtu kwani baadhi ya watalii huja mkoani Kagera wakitokea ng’ambo ili pengine kuona maeneo ambayo babu au baba zao waliwahi kufanyia kazi wakati wa ukoloni. Alipoulizwa ni vivutio gani ambavyo ameshuhudia kuweza kuwakosha zaidi watalii wan je ya nchi wafikapo Kagera  aliongeza kuwa ni mashamba ya chai ambapo wao husema kuwa wao huliona tu zao la chai madukani huko kwao lakini kuwa hawajawahi kuliona zao hilo likiwa limeoteshwa shambani.Watalii hupenda sana kupiga picha wakati wakiwa wanaigiza kuvuna chai katika mashamba hayo.
(itaendelea toleo lijalo)

Yapo matatizo yanayoikabili sekta ya utalii mkoani Kagera kama vile hali ya usalama katika mapori ya Biharamulo,Ngara na Karagwe hali ambayo bado inahitaji kudhibitiwa zaidi na huku watalii wakihakikishiwa usalama wawapo ndani ya maeneo hayo.Kutokuwepo kwa uwanja wa ndege wa uhakika hususan wa kimataifa ambao pengine ungeliwasaidia hata mikoa ya nchi jirani ipakanayo na mkoa wa Kagera nayo pia ni Changamoto.Ni busara mradi wa kufikirika wa kutaka kuujenga uwanja huo katika maeneo ya Omukajunguti ukatekelezwa bila kusita.

Mkoa wa kagera hakika unasheheni vivutio vingi ambavyo vingine bado havijabainishwa au hata kutangazwa vya kutosha.Mto Kagera ni chanzo cha mto Nile ambapo duniani kote hamna watu wasiousikia au kuusoma vitabuni mto huo mashuhuri  duniani.Wapo aina wa ndege tofauti tofauti katika vituo vya kuwashuhudia ndege hao na vijito lukuki ambapo watalii wanaweza kufurahia ulowaji samaki ndani ya vijito hivyo pia ypo maji moto Mutagata ya huko wilayani Karagwe.

Alipowasiliana na viongozi wa kampuni(Kiroyera tours) inayoendesha shughuli za utalii mkoani Kagera mwandishi wa makala haya alielezwa jinsi kampuni hiyo inavyoendelea na jitihada za kuutangaza mkoa huo ili nao uweze kuwemo miongoni mwa maeneo maarufu kwa ujio wa watalii nchini Tanzania.

Miongoni mwa juhudi hizo ni kulitangaza ZIWA VICTORIA ambalo ni ziwa kubwa duniani ambalo maji yake siyo ya chumvi na kuwa mtalii anaweza kuingia mkoani Kagera  hatakwa kutumia meli akipitia ndani ya ziwa hilo hadi mjini Bukoba.BUKOBA ni mji unaofikika kirahisi  hata kwa kutokea Nairobi,Kisumu,Mwanza,Kampala,Entebbe,Kigali,,na Bujumbura.Barabara mpya ya lami inayojengwa sasa hivi kutoka Bukoba hadi Wilayani Karagwe itawaunganisha watalii wanaotaka kwenda kuziona hifadhi za taifa za Ibanda na Burigi,majimoto ya Mutagata na kwingineko
Kwa  vile mkoa huo unaweza kufikiwa kirahisi na idadi kubwa ya watalii wanopita kwenda au kutoka nchi jirani ni dhahiri sana iwapo vivutio vile ambavyo bado havijabainishwa vikabainishwa ili watalii hao wakachelewa mkoani humo ili matumizi yao yakahitimishwa mkoani humo pia.
Mkoani Kagera zipo ngoma na michezo asilia kama vile Omutooro,Akasimbo,kutupa mkuki,kuvuta kambangoma za akina mama na nyinginezo.Kwa kuwani jukumu la idara ya Utamaduni kviendeleza vipaji vya aina hiyo,sasa ni wakati wa kuifanya kazi hiyo katika kuwaandaa wananchi wakavuna fedha za watalii pindi waingiapo mkoani humo.

Zoezi endelevu la kuuweka safi mji wa Bukoba a miji mingine ya mkoa wa Kagera chini ya Uongozi wa mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabian Massawe ni jambo la kujivunia sana mintarafu sekta ya utalii nchini.Mtalii ni mgeni wa mahali hivyo ni jambo linalosikitisha mno iwapo mgeni huyo anaikuta nyumba yetu ni chafu na haitamaniki.

Kwa hali hiyo panahitajika juhudi zaidi za wananchi hata kuyapiga rangi za kupendeza majengo yetu huku tukiendelea zaidi kuyaboresha mazingira tuishimo.Tunaelezwa na wamiliki wa makampuni ya utalii mkoani Kagera kuwa wageni wanaoutembelea sana mkoa huo ni hasa kutokea nchi za ulaya kaskazini na Afrika kusini. Huko vijijini kwa wale wananchi ambao bado wanazitunza nyumba za asili maarufu kama “MUSHONGE” waendelee kuzihifadhi nyumba hizo kwani huenda hicho kikawa kivutio maalum ambacho bado hakijaainishwa baraabara,kwani utalii si lazima ukaishia mijini tu.